Sura za Habari Hii |
---|
Mbunge: Kuna unafiki CCM |
Madai ya kununuliwa Lowassa |
Habari Yote |
*Yadaiwa kuwa atashitakiwa kwa Kikwete, Kinana
*Adai kuwa hiyo ni sumu hatari ndani ya chama hicho
MBUNGE wa Jimbo la Mwibala (CCM), Kangi Lugola, amesema tuhuma dhidi yake kuwa anakidhoofisha chama chake bungeni hazina msingi wowote, na kamwe haziwezi kumtisha.
Lugola alitoa kauli hiyo katika mahojiano na Rai Jumanne wiki hii, baada ya kuwapo taarifa za yeye na wabunge wengine wawili kushitakiwa kwa Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana, kutokana na mwenendo wao wa kuikosoa Serikali bungeni.
Mbali ya kuwapo taarifa za wabunge hao kushitakiwa kwa Katibu Mkuu wa CCM, taarifa nyingine zimedai kuna mkakati mkubwa wa kuwashughulikia katika kikao kinachotarajiwa kufanyika wiki chache zijazo kati ya Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete na wabunge wa chama hicho mjini Dodoma.
Mbali ya Lugola, wabunge wengine wanaonyoshewa vidole ni Deo Filikunjombe wa Jimbo la Ludewa na Luaga Mpina wa Jimbo la Kisesa.
Akizungumza kwa kujiamini, Lugola alisema; “Kuna wabunge wa CCM wenye dhana potofu kabisa, wao wanadhani au kufikiri kuwa Mbunge anayetokana na chama chetu hapaswi kuhoji Serikali yake suala lolote linalohusiana na utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi.
“Dhana hii potufu inaambatana na woga na unafiki, ndio sababu wale ambao tunaikosoa Serikali kwenye mambo ya msingi kwa lengo la kuisaidia na wakati huo huo kuimarisha chama, tunaonekana tatizo.
“Dhana hii inapandikiza sumu hatari miongoni mwa viongozi na wanachama, na matokeo ya sumu hii mbaya ni kuzaa chuki na fitina, jambo ambalo ndilo linalotokea sasa miongoni mwa wabunge.
“Hali hii ikiachiwa bila kukomeshwa kwa vitendo na si maneno, chama kitadumaa, kitakuwa legelege na matokeo yake ni kuzaa au kuwa na Serikalu legelege.
“Ndio maana kuna wabunge wenye fikra chanya ambao hawataki Chama Cha Mapinduzi kifike huko, matokeo yake ni msuguano unaoonekana sasa.
“Hizi habari za kushitakiwa kwa uongozi wa juu wa chama hazininyimi usingizi kwa sababu ni maoni ya mtu, watu au wabunge wanafiki wenye ajenda zao binafsi.
“Siamini kama CCM ninayoifahamu na inayofahamika kwa Watanzania inaweza kukaa chini kujadili na hatimaye kukubaliana na wabunge wanafiki.
“Serikali au chama bila kukosolewa kitabweteka, kwa mimi na baadhi ya wabunge wenzangu ambao tunaonekana kuwa wasaliti si wasaliti, bali tunachofanya ni kukiimarisha chama, na kuifanya Serikali itimize wajibu wake kwa wananchi.
“Hata Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere, ambaye ndiye Baba wa CCM, aliwahi kusema wana-CCM wasisite kukosoana na kusahihishana, sasa kosa letu hapa ni lipi? Hivi tangu lini kukosoana kukakidhoofisha chama?
Maoni
wana ccm hiyo ni dalilil nzuri ya demokrasia kukua nchini na ukomavu wa sisa