Rai

  • Increase font size
  • Default font size
  • Decrease font size

Rai

Mbunge: Kuna unafiki CCM

Print PDF

*Yadaiwa kuwa atashitakiwa kwa Kikwete, Kinana
*Adai kuwa hiyo ni sumu hatari ndani ya chama hicho

MBUNGE wa Jimbo la Mwibala (CCM), Kangi Lugola, amesema tuhuma dhidi yake kuwa anakidhoofisha chama chake bungeni hazina msingi wowote, na kamwe haziwezi kumtisha.

Lugola alitoa kauli hiyo katika mahojiano na Rai Jumanne wiki hii, baada ya kuwapo taarifa za yeye na wabunge wengine wawili kushitakiwa kwa Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana, kutokana na mwenendo wao wa kuikosoa Serikali bungeni.

Mbali ya kuwapo taarifa za wabunge hao kushitakiwa kwa Katibu Mkuu wa CCM, taarifa nyingine zimedai kuna mkakati mkubwa wa kuwashughulikia katika kikao kinachotarajiwa kufanyika wiki chache zijazo kati ya Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete na wabunge wa chama hicho mjini Dodoma.

Serikali yaendeleza ahadi kwa wafanyakazi

Print PDF

SERIKALI imeendeza ahadi zake kwa wafanyakazi nchini kwamba itajitahidi kuyatatua matatizo wanayokumbana nayo na kuboresha maslahi yao kadri inavyowezekana.
Akizungumza kwenye maadhimisho ya Sikukuu ya Wafanyakazi (Mei Mosi) jijini Mbeya jana, Rais Jakaya Kikwete alisema Serikali haiwezi kupandisha ghafla mishahara, bali itafanya hivyo hatua kwa hatua kadri inavyowezekana.

Mengine yaanikwa kampuni ya Bakhresa

Print PDF

SIKU chache baada ya wafanyakazi wa Kampuni ya Said Salum Bakhresa, kutoa malalamiko kuhusu unyanyaswaji wanaofanyiwa , tuhuma nyingine zimezidi kuibuliwa. Tuhuma hizo zinakihusu kiwanda cha kutengeneza mikate kilichopo eneo la Kipawa jijini Dar es Salaam. Wakizungumza na RAI wafanyakazi hao na wengine ambao wamedai kufukuzwa kazi kwa ajili ya kutetea maslahi yao walisema kiwanda hicho kinaendeshwa kibabe.

Wabunge wetu na ushindani wa maneno

Print PDF

NI dhahiri kuwa wabunge wetu wamechoka kiasi kwamba hawatoi tena mawazo yaliyo makini. Baadhi yao wakiongea wanapwaya tu hasa katika uchangiaji wa kuifanya nchi isonge mbele. Jambo la kusikitisha ni kwamba mbunge anapopewa muda wa kuzungumza husimama bila hoja ya msingi, mpaka dakika alizopewa na Spika humalizika bila kujua alikuwa anachangia jambo gani la muhimu kwa mustakabali wa taifa.

ITV, Star TV kwanini mnatuonyesha maiti?

Print PDF

MWANGWI WA LYAMBA-LYA-MFIPA
*Museveni naye ni wale wale!
HAKIKA picha za mikutano ya CCM na CHADEMA nilizoziandikia makala wiki iliyopita zimenipa fundisho kubwa nawashukuru wadau wa safu hii walionipigia simu na wengine kuniandikia ujumbe.

Kurasa 5 kati ya 34

Waliotutembelea