*Yadaiwa kuwa atashitakiwa kwa Kikwete, Kinana
*Adai kuwa hiyo ni sumu hatari ndani ya chama hicho

Mbunge wa Mwibara (CCM), Kangi Lugola
Lugola alitoa kauli hiyo katika mahojiano na Rai Jumanne wiki hii, baada ya kuwapo taarifa za yeye na wabunge wengine wawili kushitakiwa kwa Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana, kutokana na mwenendo wao wa kuikosoa Serikali bungeni.
Mbali ya kuwapo taarifa za wabunge hao kushitakiwa kwa Katibu Mkuu wa CCM, taarifa nyingine zimedai kuna mkakati mkubwa wa kuwashughulikia katika kikao kinachotarajiwa kufanyika wiki chache zijazo kati ya Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete na wabunge wa chama hicho mjini Dodoma.